Rais akubali kujiuzulu kwa
Chenge
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo
April 20, 2008, amepokea barua kutoka
kwa Waziri wa Miundo Mbinu, Mheshimiwa
Andrew Chenge ya kujiuzulu wadhifa wake na Rais amekubali ombi
Rais ameuelezea uamuzi huo wa
Mhe Chenge
Katika barua yake kwa Rais, Mhe Chenge amesema kuwa pamoja na
kwamba shutuma dhidi yake bado zinachunguzwa, mapenzi yake kwa nchi na chama
chake, yamemsukuma kujiweka pembeni. Mhe Chenge ni Mbunge wa Bariadi Magharibi.
Mwisho
Imetolewa na Ikulu,
20th April, 2008