UNITED
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tanzania
imeteuli kuwa moja ya nchi TANO katika
kamati ya Umoja wa Afrika kutafuta
ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Ivory Coast kati ya Rais anayemaliza muda wake
Bwana Laurent Gbagbo na Bwana Alassane Outtara.
Nchi zingine
kaatika kamati hiyo ni Chad, Mauritania, Nigeria na Afrika ya Kusini, nchi hizi
zitaungana na nchi ya Burkina Faso ambayo tayari inashughulikia mgogoro huo.
Kamati hiyo
imefanya mkutano wake wa kwanza jana jioni tarehe 31, Januari 2011 mjini Addis Ababa ambapo
imekubaliwa kuwa kila nchi itachagua mwakilishi wake katika kamati ndogo ya
wataalamu ifikapo tarehe 3 Februari ambao watakwenda nchini Ivory Coast
kuangalia na kutathmini hali ilivyo.
Baada ya hapo
Kamati ya wataalamu watatakiwa kutoa taarifa na ushauri kwa viongozi ambao hatimaye watakwenda Ivory
Coast na kukutana na viongozi hao wawili wanaogombea madaraka.
Wakati huo huo
Rais Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Maendeleo na
Ushirikiano wa Kimataifa Bwana Adrew Mitchell.
Katika
mazungumzo yao Bwana Mitchell amemhakikishia Rais Kikwete kuwa Uingereza itaendelea
kuisaidia Tanzania katika bajeti yake na pia katika sekta mbalimbali ikiwemo
elimu na afya.
Katika
mazungumzo yao, viongozi hao kwa pamoja wamekubaliana kwa pamoja kufanya kazi itakayoonyesha
mafanikio na majibu yatakayoleta
manufaa kwa watu wake.
Rais Kikwete
amemweleza Waziri Mitchell dhamira yake ya kuongeza jitihada katika kukuza
elimu nchini na kuongeza upatikanaji wa huduma ya afya kwa wananchi karibu na
makazi yao.
Waziri
Mitchell amesema Uingereza itamsaidia na kushirikiana na Rais Kikwete katika
kutimiza azma yake hiyo ambapo wataongeza msaada zaidi katika sekta hizo muhimu
za elimu na afya nchini Tanzania.
Rais Kikwete
anatarajiwa Kurejea nyumbani leo mchana.
Mwisho.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa habari wa Rais, Msaidizi
Addis-Ababa
01 Februari, 2011