DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania na Mwenyekiti wa Umoja
wa Afrika, amesema Marehemu Levy Mwanawasa wa Zambia ameishi na kuwatumikia
wananchi wa Zambia kwa mapenzi, kujitolea,
heshima na kwa dhati kubwa
na wananchi wa Zambia wanaweza kumlipa hilo kwa
kumuenzi katika matendo yake haya.
Rais Kikwete amewaambia waombolezaji katika viwanja vya bunge mjini
“Ameishi maisha yake na kuwatumikia watu wake kwa mapenzi,
heshima na kwa ustaarabu, kitu mnachoweza kumrudishia ni kumuenzi, fuateni na tekelezeni yale
aliyobakiza”.
Rais Kikwete ametoa salamu hizo
kwa niaba ya viongozi wa
Afrika watu wake na Tanzania ambapo amewaambia wananchi wa Zambia kuwa Mrehemu Mwanawasa alikuwa rafiki na mwenzake kama alivyokuwa kwa viongozi wengine katika ukanda huu
na duniani kwa ujumla.
“Yeye na mimi tulipatana
sana kama ilivyo kawaida kwa viongozi wa
nchi mbili rafiki na majirani,
siku zote tulikuwa tunawasiliana na kila mara
kulipotokea jambo linalotuhusu sote tulishauriana na kwa kweli utamaduni
huu ulikwenda vizuri kwa faida
ya nchi zetu
mbili” amesema na kumuelezea kuwa
alikuwa kiongozi wa kutumainiwa na rafiki mkubwa
kwa Watanzania, nchi jirani Afrika
na dunia kwa ujumla na
kwamba Tanzania na bara la Afrika limepoteza mtu muhimu”.
Rais Kikwete amesema viongozi na waombolezaji
wamekuja kutoka karibu na mbali
na
Premi
Kibanga,
Lusaka,
Zambia
03
September, 2008