DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Serikali
ya Awamu ya Nne imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma ya
afya karibu na makazi
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete amemweleza Rais wa Zamani wa
“Lengo
letu ni kuboresha huduma ya afya kwa kuongeza huduma bora, kuboresha hospitali,
zahanati na vituo vilivyopo na pia kujenga zingine kwa lengo la kuhakikisha
kuwa huduma za afya zinapatikana si zaidi ya kilomita tano kutoka wananchi
wanapoishi” ameeleza.
Bi
Robinson ni mwanzilishi wa shirika lisilo la kiserikali la “Realising Rights”
ambalo lengo
Bi
Robinson hufanya shughuli za kuhamasisha washika dau wakiwemo viongozi wa
kiserikali, wafanya biashara na viongozi wengine katika nyanja mbalimbali
kutafuta njia na mbinu za kusaidia katika kufanikisha na kuhakikisha kuwa watu
wa kipato cha chini wanapata haki ya kupata huduma za kiafya na ajira bora.
Bi.
Robinson amewahi kuwa Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kati ya
mwaka 1997 hadi 2002 mara tu baada ya kumaliza kipindi chake cha Urais wa
Katika
kuboresha huduma hizo za afya nchini serikali itapanua na kuboresha hospitali
za wilaya, mikoa na pia kujenga na kuongeza hospitali kuu hapa nchini, kuongeza
mafunzo kwa wahudumu wa afya wakiwemo madaktari, manesi na watendaji wengine
ikiwemo pia kuwaongezea ujuzi wahudumu waliopo sasa.
Serikali
pia kwa kushirikiana na nchi marafiki, inaweka utaratibu ambapo wakunga wa jadi
watapewa mafunzo na kupewa zana za afya kwa ajili ya kuendelea kutoa huduma
mahali walipo kwa njia iliyo bora na salama zaidi.
Rais
Kikwete pia amemueleza Bi. Robinson kuhusu juhudi za serikali katika kupambana
na magonjwa hatari
Katika
jitihada hizo pia serikali inafanya juhudi kubwa katika kuhakikisha malengo ya
milenia ya kupunguza vifo vya mama na mtoto yanafanikiwa ambapo tayari hatua
kubwa imepigwa katika kuongeza idadi ya watoto wanaopata chanjo.
Pamoja
na hayo, kutokana na juhudi mbalimbali zilizokwisha fanywa kuhusu kupunguza
vifo vya mama wajawazito, serikali imeanza kufanya sensa kuona mafanikio hayo
yamefikia wapi ili kuongeza nguvu na mikakati zaidi na matokeo yake
yanatarajiwa kutoka mwishoni mwa mwaka huu.
Leo
katika Ikulu ya Dar-es-salaam, Rais pia ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri
kinachotarajia kumalizika jioni.
Mwisho
Imetolewa
na Premi Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais Msaidizi
Ikulu-DSM
08
Oktoba, 209