¨
Ofisi ya Taifa ya Takwimu
¨
Mfumo wa Kusambaza Data
¨
Chunguzi za Demografia na Afya
Tanzania
¨
Sensa ya Taifa ya mwaka 2002
¨
Kituo cha Takwimu za Uchumi na
Jamii Tanzania
¨
Mtandao wa Habari za Idadi ya
Watu Tanzania
¨
Taasisi za Takwimu Tanzania
Ofisi
ya Taifa ya Takwimu
Ofisi
ya taifa ya takwimu, kama wakala wa Serikali iliundwa kutokana na
ofisi ya zamani ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa ajili ya kutoa
huduma kwa ufanisi, ili fedha itolewayo iwe na thamani zaidi kwa
manuaa ya Serikali na wananchi kwa jumla.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu inafanya kazi zake kibiashara,
ikitumia usimamizi wa fedha wa kibiashara, na mbinu za kupanga
kibiashara, na inamwelekea zaidi mteja.
Dira
Dira
ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu, kama wanavyoiona watumishi, ni kuwa
chanzo chenye mamlaka na cha kuaminika cha habari za takwimu
ihusuyo hali ya jamii na uchumi nchini, taasisi yenye uwezo wa
kutoa taarifa inavyotakiwa, mahali pa rejea kwa methodolojia ya
takwimu na viwango, na kituo cha kuratibu shughuli za takwimu kwa
lengo la kutoa takwimu dhabiti.
Mwelekeo.
Mwelekeo
ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu, ni kuwezesha upangaji mipango na
uchukuaji maamuzi ndani ya Serikali na jumuiya ya kibiashara,
kuchochea utafiti na kuarifu umma kupitia takwimu za kuaminika na
za wakati, na kutoa huduma bora ya takwimu kwa jumla.
Ofisi
ya Taifa ya Takwimu ni wakala pekee mwenye mamlaka ya kutoa
takwimu kwa Serikali, jumuiya ya kibiashara na wananchi kwa jumla.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu inajitahidi kutekeleza wajibu huu
kwa niaba ya Serikalai kwa uadilifu na ufanisi kwa kupunguza
gharama zisizokuwa za lazima. Ina uwezo wa teknolojia wa kuweza
kutoa huduma ya takwimu kwa Taifa.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu iko tayari kukabiliana na
changamoto yeyote katika utoaji wa huduma hii kwa kupunguza
gharama za uendeshaji, na kugharamia shughuli zake kwa kuweka bei
za kuvutia za bidhaa na huduma zitolewazo.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imedhamiria kutoa huduma za
takwimu nchini.
Anwani
Ofisi
za Takwimu ziko Jengo la Casino Mtaa wa Kivukoni Front.
S.L.P.
796
DAR
ES SALAAM.
Simu:
255-22-2122722/3/4/5/,. 2137834, 2111634
Fax:
2112352
Baruapepe:
nbs.dg@raha.com
Website:
www.nbs.com.tz