Tanzania Kiufupi

Nchi ya Tanzania iko katika pwani ya Mashariki ya Bara la afrika kati ya longitudo 29 na 41 Mashariki, na Kati ya latitudo l na l2 kusini.  Ncha ya kaskazini kabisa ya nchi ni mji wa Bukoba, usawa wa latitudo l Kusini; na ncha ya Kusini kabisa ni mji wa Mtalika, usawa wa latitudo 12 kusini.  Ncha ya Magharibi kabisa ni mji wa kigoma usawa wa longitudo 29 mashariki ya msistari wa Greenwich, na ncha ya Mashariki kabisa ni mji wa Mtwara ulioko usawa wa Longitudo 41.

 

Kwa upande wa kaskazini, Tanzania imepakana na nchi za Kaenya na Uganda ambapo upande wa magharibi imepatana na nchi za Burundi na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.  Kwa upande wa kusini, Tanzania imepakana nchi za Zambia, Malawi na Msumbiji ambapo upande wa mashariki imepakana na Bahari ya Hindi.

 

·        Mazingira ya Nchi:

 

Tanzania ndiyo nchi kubw akupita nchi zote za Afrika mashariki (Kenya, Uganda na tanzania).  Tanzania ina maumbile matatu ya kipekee ambayo ni Visiwa vya Zanzibar na Pemba na Ukanda wa pwani kwa upande wa mashariki, na muinuko wenye umbile la bakuli katikakakati, pamoja na nyanda za juu.  Bonde la ufa (The Greaf Rift Valley) ambalo LINAANZIA Kaskazini-Mashariki ya Bara la Afrika na kupitia katikati ya Tanzania ndiyo alama nyingine kubw inayoongeza mandhari ya nchi.  Bonde hilo la ufa limekwenda hadi kufikia kusini katika Ziwa Nyasa na kujigawa pande mbili, moja ikiendelea Kusini zaidi ya Ziwa Nyasa hadi Mozambique, na pande nyingine ikielekea Kaskazini-Magharibi pembezoni mwa Burundi, Rwanda, Tanzania na sehemu ya Magharibi ya nchi ya Uganda.

 

Ndani ya Bonde Kuu hili la ufa, kuna msururu wa maziwa kama vile Ziwa Rukwa, Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa, Ziwa Kitangiri, Ziwa Eyasi na Ziwa Manyara.  Sehemu za miinuko ni pamoja na Kipengere, Udzungwa, Matogoro, Livingstone na Ufipa ambazo kwa pamoja zinafanya Nyanda za Juu za Kusini.  Safu ya milima ya Usambara, Pare, Meru, Kilimanjaro, Shimo la Volkeno la Ngorongoro na Oldonyo Lengai vyote hivi ndivyo vinavyoitwa Nyanda za Juu za Kaskazini.  Kutoka shemu hizi za miinuko pamoja na bonde la Kati ndiko kunakopita mitiririko ya maji ambayo hatimaye huishia katika bahari za Hindi, Atlantic na Mediterranean pamoja na maziwa na mabwawa yaliyomo nchini.

 

Milima ya Tanzania:

 

-                     Mlima Kilimanjaro wenye urefu juu ya usawa wa bahari wa mita 5,895

-                     Mlima Meru, mita 4566

-                     Mlima Rungwe, mita 2,960

-                     Milima ya Uluguru, mita 2,648

-                     Milima ya Rubeho, mita 2,576

-                     Milima ya Livingstone, mita 2,521

-                     Mlima Mbizi, mita 2,418

-                     Mlima Mahari, mita 2,373

-                     Milima ya Usambara, mita 2,300

 

Hali ya Hewa:

 

Nchi ya Tanzania ni ya hali ya joto (tropical type of climate).  Katika nyanda za juu hali ya joto inaanzia nyuzi joto 10 hadi 20 wakati wa baridi na joto.  Sehemu nyingine zilizobakia nchini joto lake mara nyingi halipungui chini ya nyuzi joto 20.  Kipindi chenye joto kali ni kati ya mwezi Novemba na Februari (Nyuzi joto 25-31) na kipindi cha baridi kali ni kuanzia mwezi Mei hadi Agosti (Nyuzi joto 15-20).  Kuna misimu miwili ya mvua katika Tanzania.  Msimu wa kwanza ambao una mvua fupi peke yake unaanzia mwezi Desemba hadi Aprili; na msimu mwingine wenye mvua fupi na ndefu ni kati ya Mwezi Oktoba na desemba, halafu kati ya Machi na Mei.

 

Katika msimu wa pili, mvua za mwezi Machi hadi Mei zinaitwa mvua za masika (mvua ndefu) wakati zile za miezi ya Oktoba hadi desemba zinajulikana kwa jina la mvua za vuli, au mvua fupi.

 

Maelezo kuhusu Tanzania:

 

·        Eneo:

 

Tanzania nzima ina eneo la nchi kavu la kilomita za mraba 945,000 ambazo kati ya hizo, Kilomita za mraba 881,000 ni eneo la Tanznaia Bara peke yake, na kilomita za mraba 2,000 ni eneo la visiwa vya Zanzibar na Pemba.  Eneo lililofunikw ana maji kwa nchi nzima ni Kilomita za mraba 62,000 na eneo la mwiktu na pori ni kilomita za mraba 3,350.

 

·        Mfumo wa Siasa:      Dekokrasia ya vyama vingi

·        Utawala:  Kuna mikoa ya utawala 25 (Bara 20 na Zanzibar 5), wilaya za utawala 123 (Zanzibar 10 na Bara 113).

·        Idadi ya Watu:  Tanzania nzima inakadiriw akuwa na jumla ya watu milioni 32 (makisio ya mwaka 2001).  Kati ya idadi hiyo yote, asilimia 51 ni wanawake na asilimia 46 ni watoto walio na umri chini ya miaka 15.

·        Umasikini:  Takriban asilimia 50 ya idadi ya watu wote nchini wanaishi maisha ya ufukara.

·        Pato la Taifa kwa mtu mmoja:  Dola za Kimarekani 246 (mwaka 2001).

·        Pato la Ndani ya nchi kwa mtu mmoja:  Dola za Kimarekani 251 (mwaka 2001).

 

Maliasili

 

·        Madini – dhahabu, almasi, tanzanite, mawe mengine ya thamani, gesi ya asili, chuma, mkaa wa mawe, maji ya chemchem, nta ya kung’ara, magadi na chumvi.

·        Wanyama na Utalii:  Mbuga 12 za wanyamak, Eneo la Hifadhi la Ngorongoro, Hifadhi za wanyama 13, Hifadhi maalum za wanyama 38 na sehemu za hifadhi za utamaduni 120.

·        Uvuvi: 

Hufanyika kwenye maziwa makuu matatu ambayo ni Victoria, Tanganyika na Nyasa pamoja na mito na pwani ya Bahari ya Hindi. Pato la samaki linaloweza kupatikana kwa mwkaa mzima linakadiriw akuwa tani za metriki 730,000 kwa mwaka, ingawa kwa hivi sasa ni tani 350,000 tu kwa mwaka.

 

Mji Mkuu:

 

Dodoma ndiyo mji mkuu na Makao makuu ya Serikali ya Tanzania.  Mji huu, wenye idadi ya watu wapatao 300,000 (Makisio ya mwaka 1998), uko umbali wa kilomita 309 kutoka dar es Salaam kuelekea mashariki.  Dar es Salaam ndiyo mji mkuu wa kibiashara.  Miji mingine mikubw ani Arusha, Moshi, Tanga na Mwanza kwa upande wa Kaskazini ya nchi, Moarogoro upande wa Mashariki; Mbeya na Iringa upande wa Magharibi.  Tabora na Shinyanga pia ni miji maarufu kwa shughuli za kiuchumi nchini Tanzania.  Dar es Salaam na Mwanza ndiyo pekee yenye hadhi ya jiji.

 

Sikukuu za Kitaifa (2002)

 

1    Januari            -            Mwaka Mpya

12  Januari            -            Mapinduzi Zanzibar

11    Machi            -            Idd - Eli - Hadji (yategemea kuandama kwa mwezi)

29   Machi            -            Ijumaa Kuu

1   Aprili                -            Jumatatu ya Pasaka

26   Aprili              -            Muungano wa Tanzania

1     Mei                -            Siku ya Wafanyakazi Duniani

27     Juni            -            Maulid (inategemea kuandama kwa mwezi)

7     Julai             -            Sabasaba

8     Agosti          -            Siku ya Wakulima

9     Desemba          -            Uhuru na Jamhuri  

5 na  Desemba     -         Idd - El - Fitri (inategemea kuandama kwa mwezi)

25   Desemba            -         Kuzaliwa Kristo

26   Desemba            -         Siku ya Kupeana Zawadi

 

Alama za Taifa

 

·        Bendera ya Taifa:

 

Uwiano wa urefu na upana:-      Tatu kwa mbili, mfano ft.3xft.2, ft.6xft.4, ft. 12xft.8.

Ina rangi za kijani, dhahabu, nyuekusi na bluu, ambapo rangi nyeusi imepit katikati ya bendera kuanzia pembe ya chini kwenye mlingoti na kuishia pembe ya juu kulia.  Rngi hii huigawa bendera katika sehemu mbili zenye umbo la pembe tatu. Rangi nyeusi imetenganishwa na pembe tatu ya juu yenye rangi ya kijani na pembe tatu ya chini yenye rangi ya bluu kwa mistari miwili midogo yenye rangi ya dhahabu.

 

Viwango vya rngi na maana zake:-

 

Nyeusi       -           Kiwango Na. 9-103       - maana yake ni WATU .

Kijani      -           Kiwango Na. 0-010      - maana yake ni ARDHI

Bluu      -           Kiwango Na. 0-012      - maana yake ni BAHARI na MAZIWA

Dhahabu       -           Kiwango Na. 0.002      - maana yake ni madini

 

Uwiano wa rangi:

 

Rangi nyeusi kwa bendera ya Ft. 6xft.4 ni 13/18 kwenda juu n13 upana.  Mistari ya dhahabu ni 1/16 kwenda juu na inchi 3 upana kila mmoja.

 

·        Wimbo wa Taifa

 

(1)               Mungu ibariki Afrika

Wabariki viongozi wake

Hekima, umoja na amani

Hizi ni ngao zetu

Afrika na watu wake.

 

KIBWAGIZO

 

Ibariki, Afrika

Ibariki, Afrika

Tubariki, watoto wa Afrika.

 

(2)               Mungu ibariki Tanzania

Dumisha uhuru na umoja

wake kwa waume na watoto

Mungu, ibariki

Tanzania, na watu wake.

 

KIBWAGIZO

 

Ibariki, Tanzania

Ibariki, Tanzania

Tubariki, Watoto wa Tanzania

 

Title

.

Title

.

Title

.