Uchukuzi

Sekta ya usafirishaji ina mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na uchumi Tanzania.  Sekta imeendelea kukua kutokana na juhudi za uwekezaji wa Serikali pamoja na sekta binafsi katika kukarabati barabara, kukuza mawasiliano ya simu, kufanya bandari kuwa za kisasa na uboreshaji wa huduma za usafiri majini, reli na anga.

Usafiri wa reli.

Mifumo miwili ya reli inatumika Tanzania.  Shirika la Reli Tanzania lina njia mbili: njia ya kati inayoanzia Dare es Salaam hadi Tabora na kugawanyika kwenda Kigoma kwa upande wa magharibi kwenye Ziwa Tanganyika, na hivyo kutoa huduma ya usafirishaji mizigo kwa eneo hilo kwa nchi za Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.  Tawi la pili ni lile la kwenda Mwanza kwenye bandari ya Ziwa Viktoria, ikitoa pia huduma ya usafirishaji mizigo kwa eneo la kaskazini na kaskazini-magharibi, ikiwemo Uganda.  Njia ya pili ni ile ya kutoka Ruvu kuelekea kaskazini hadi Korogwe, na kugawanyika kwenda Tanga kwenye bahari ya Hindi na kaskazini –magharibi hadi Moshi kuunganisha na mfumo wa reli ya Kenya.

Mfumo mwingine wa reli ni, reli ya Mamkala ya Reli Tanzania na Zambia- TAZARA.  Hii ni reli ya pamoja ya nchi za Tanzania na Zambia.  TAZARA inaunganisha bandari ya Dar es Salaam na Zambia ikisafirisha mizigo ya nchi za Malawi, Zimbabwe, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Zambia.  Shirika la Reli Tanzania na Mamlaka ya Reli ya Tanzania-Zambia yamepangwa kubinafsishwa.

Usafirishaji Majini

Mamlaka ya Bandari Tanzania inasimamia bandari za Dar es Salaam, Tanga Mtwara na Bandari ndogo za Kilwa na Lindi kwenye Bahari ya Hindi.  Dar es Salaam ndiyo bandari kubwa yenye uwezo wa kusafirisha mizigo mingi.

Kuna usafirishaji wa maziwa unaoendeshwa na Idara ya Majini ya Shirika la Reli Tanzania.  Kuna huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo katika Ziwa Victoria (kuunganisha Tanzania, Kenya, Uganda), Ziwa Tanganyika (kuunganisha Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Zambia), na kwenye ziwa Nyasa (kuunganisha Tanzania, Malawi, Msumbiji).

Usafiri wa Anga

Tanzania ina viwanja vya ndege vya kimataifa vitatu:  Dar es salaam, Kilimanjaro na Zanzibar.  Zaidi ya hivyo kuna viwanja vingine vya ndege vilivyoenea nchini nzima.  Shirika la Ndege la Taifa – ATC ni msafirishaji mkuu ndani ya nchi likiunganisha miji yote mikubwa nchini.  Kampuni binafsi nazo zimeanza kutoa huduma ya kusafirisha abiria, na pia kuna kampuni za ndege za kukodi.  ATC ina huduma nchi za jirani na Mashariki ya Kati. Pia kuna ndege za mashirika ya kimataifa zenye kusafiri kati ya Tanzania na Ulaya, India, Mashariki ya Kati na Kusini mwa Afrika.

Usafiri wa Barabara

Jiolojia ya Tanzania, ukubwa wake, uanuwai na mtawanyiko unaipa nafasi kubwa barabara katika kuunganisha uchumi wa Taifa.  Na hasa barabara huhudumia vijijini (wanakoishi Watanzania wengi) kwa manufaa zaidi kuliko aina nyingine za usafiri.

Mfumo wa taifa wa barabara (chini ya Wizara ya Ujenzi) unakabiliana na ukosefu wa fedha za kukarabati na kuendeleza barabara kutokana na wingi wa magari (k.m. mpango wa dharura wa kukarabari barabara uliobuniwa – URRP), na kwa ajili ya matengenezoya kawaida, uwezo mdogo wa tasnia ya ujenzi, na ushiriki mdogo wa sekta binafsi.

Hata hivyo Serikali imerazinisha na kuweka pamoja mfumo wa kitaasisi wa kusimamia sekta ili kuleta ufanisi, utendaji utakiwao na uwajibikaji. Wakala unaojitegemea, Wakala wa Barabara Tanzania, (TANROADS), ulio na jukumu la kusimamia ujenzi wa barabara kuu, ukarabati na matengenezo, umeanzishwa.

Bodi ya Taifa ya Babaraba yenye wakilishi kutoka sekta binafsi, watumiaji na Serikali, husimamia shughuli za wakala hii.  Pia Serikali imeanzisha Mfuko wa Babaraba ambao mapato yake makuu hutoka kwa watumiaji wasioweza kukwepa ulipaji wake, kama chanzo kikuu cha fedha za matengenezo ya barabara.  Serikali za Mitaa chini ya Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ndiyo inayowajibika na barabara za Wilaya, za Miji na za viungo zenye kuunganisha maeneo muhimu ya uzalishaji kilimo vijijini,  uchimbaji mdogo mdogo wa madini, na utalii vijijini.

Title

.

Title

.

Title

.