|
Katika jitihada za kuimarisha mazingira
ya uwekezaji nchiniTanzania,
Serikali hivi karibuni iliamua kupitia upya Sera ya Uwekezaji
Tanzania ya February, 1990. Sera mpya ya Uwekezaji ilipitishwa na
serikali mwezi Oktoba, 1996.
Sera mpya ya uwekezaji
inatilia mkazo mambo yafuatayo:
·
Uhasishaji na matumizi ya kiwango cha juu cha rasilimali za hapa nchini,
ikiwa ni pamoja na kushirikiana na nchi nyingine zinazoendelea na
nchi zenye viwanda.
·
Kuongeza mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi, ili kuendeza sekta ya
biashara ya nje.
·
Kuhamasisha mitaji kutoka nje ya nchi kwa lengo la kuimarisha juhudi za
Taifa
·
Kuhimiza matumizi ya technolojia mpya katika shughuli mbalimbali hasa
zile zenye uhusiano wa moja kwa moja na uongezaji tija, ubora na
ushindani katika biashara.
¨
Kuongeza uwazi katika mfumo wa Sheria ambako kutasaidia kuinua na
kulinda rasilimali zote zilizowekezwa
·
Kuondoa vikwazo vya kupata vibali vya kuwekeza nchini
·
Kuchambua wajibu za sekta binafsi ili kuipatia wajibu mkubwa zaidi
·
Kuoanisha taratibu za kiutawala na mfumo wa masoko kama njia ya kugawa
rasilimali
·
Kuimarisha demokrasia ya vyama vyingi vya siasa .
·
Kuimarisha Utawala wa Sheria.
Dhamana
ya Uwekezaji na Utatuzi wa Migogoro
Mali za wawekezaji nchini Tanzania zinalindwa na sheria dhidi ya
utaifishaji na uporaji. Tanzani ni mwanachama wa Vyama viwili vya
kimataifa vinavyoshughulikia migogoro ya mali za wawezekaji
zilizotaifishwa ambavyo ni “International Centre for Investment
Disputes” na “Multilateral Investiment Guarantee Agency”
(MIGA). Mgogoro
wowote kati ya serikali na wawekezaji lazima kwanza usuluhishwe
kwa kutumia majadiliano au kupeleka kwa usuluhishi katika vyombo
vilivyotajwa hapo juu..
Uhamishaji
wa Mitaji na Faida
Sheria zinaruhusu bila masharti kupitia Benki yeyote iliyoruhusiwa
kuhamisha faida, kulipa madeni ya nchi za nje, ada, mrahaba au
malipo yoyote yanayohusiana na teknolojia kutoka nje ya nchi, na
malipo ya mishahara na mafao mengine ya wafanyakazi wa mataifa
mengine wanaofanya kazi Tanzania.
Mikataba
ya Uhamishaji wa Teknolojia
Hakuna vikwazo kwa makampuni kuhamisha teknolojia. Lakini kila Mkataba
wa kuhamisha Teknolojia lazima usajiliwe na kituo cha Kusimamia
Uwekezaji mara baada y a kukamilika.
Upatikanaji
wa Mikopo kwa
Wawekezaji Wageni Kutoka Taasisi mbalimbali za Kitanzania
Kampuni yoyote inayofanya kazi Tanzania inaweza kupata mkopo kutoka
Taasisi za Fedha za hapa nchini kwa mujibu wa viwango wilivyowekwa
na Benki Kuu ya Tanzania.
Sheria
na Taratibu za Ajira
Tafadhali
wasiliana na:
Idara ya Kazi Makao Makuu
Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana na Michezo
S.L.P. 9014
Dar es Salaam
Simu: 255 – 022
2110218/2110219
Fax: 255
– 022 2112045
Mtu wa kuwasiliana naye:
Kamishna wa Kazi
Sheria
muhimu kuhusu ajira ni kama zifuatazo
Kima
cha chini cha Mshahara
Mwongozo kwa Wawekezaji
Nyanja za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Bara zimegawanywa katika
sehemu mbili muhimu:
Sekta
Kuu
Uchimbaji madini, miundombinu (ujenzi wa barabara, madaraja, viwanja vya
ndege, uzalishaji wa umeme, njia za mawasiliano ya simu, huduma za
maji, na huduma nyingine za kusaidia uchimbani wa madini) na
usafirishaji wa mazao na huduma nje yz nchi.
Sekta
zinazopewa kimbaumbele
Kilimo ikiwa ni pamoja na ufugaji, usafiri wa ndege, majengo ya
biashara, Benki za Biashara, Kusafirisha bidhaa nje ya nchi,
Maendeleo ya Nguvu kazi, Viwanda,
mali asili ikiwa ni pamoja na uvuvi,
ukarabati na upanuzi, Utangazaji wa Redio na Televisheni,
Utalii na Safari za Kitalii
Motisha Kwa Wawekezaji
Tanzania inatoa motisha kwa wawekezaji waliochagua kuwekeza hapa nchini.
Motisha hizi
zimekusudiwa
§
Kuwanufaisha wawekezaji kwa uamuzi wao wa kuwekeza hapa nchini
§
Kuendana na mabadiliko ya mahitaji ya nchi
§
Kuelekeza rasilimali katika mikondo inayohitajika sana kwa maendeleo ya
kiuchumi
§
Kupunguza pengo kati ya masikini na tajiri nchini
Motisha ya kodi kwa wenye vyeti vya kuwekeza vinavyotolewa na Kituo cha
Uwekezaji na wawekezaji wengine
Sekta Kuu ( katika
asilimia %)
Kituo
Cha Uwekezaji Tanzania
Kituo
cha Uwekezaji Tanzania ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa chini
ya Sheria ya Uwekezaji Tanzania Na 26 ya mwaka 1997
kusimamia, kuratibu na
kusaidia uwekezaji
nchini. Kituo hiki ni muhimu kwa wawekezaji wote na kinafanya kazi
ya mawasiliano kwa niaba ya wawekezaji kutoka hatua za hawali
mpaka kukamilika na
kuanza kwa mradi unaokusudiwa.
Idara na Taasisi za serikali zinatakiwa kwa mujibu wa
sheria kushirikiana na kikamilifu na kituo hiki katika kusaidia
wawekezaji.
Kituo
hiki kinashughulika na makampuni yenye mtaji usiopungua Dola za
Kimarekani laki tatu (US $
300,000) kwa yanayomilikiwa na wageni na dola za Kimarekani laki
moja (US $ 100,000) yanayomilikiwa na wazawa. Makampuni
yanayojishughulisha na uchimbani wa madini na biashara ya mafuta
ya petroli, yanatakiwa kufuta taratibu za kupata vibali kama
ilivyo katika sheria zinazohusika. Hata hivyo, kituo cha uwekezaji
kinaweza kuwasaidia wawekezaji wote katika kupata ruhusa na vibali vinavyohitajika chini ya sheria nyinginezo
kuanzisha shughuli za uwekezaji nchini.
Shughuli
za Kituo cha Uwekezaji
Kituo
kinajishughulisha na
Ø
Kuanzisha na kusaidia hatua zinazoweza kuweka mazingira mazuri ya
uwekezaji nchini kwa wawekezaji wa hapa nchini na nchi nzuri
Ø
Kutafuta, kukusanya, kuchanganua na kusambaza taarifa kuhusu nafasi za
uwekezaji na njia za kupata mitaji ya kuwekeza, na kuwashauri
wawekezaji, endapo wataomba, juu ya upatikanaji, uteuzi, au uzuri
wa washirika katika miradi ya pamoja.
Ø
Kuanisha maeneo ya kuwekeza, mashamba, au ardhi na vilivyomo, mashamba
au ardhi kwa ajili ya wawekezaji na uwekezaji kwa jumla.
Ø
Kuwasaidia wawekezaji wote, pamoja na wale ambao hawabanywi na Sheria ya
Uwekezaji ya Tanzania ya mwaka 1997, kupata vibali vyote muhimu,
leseni na idhini, ruhusa, usajili na mambo mengine yanayohitajika
kwa mujibu wa sheria ili mtu aweze kuanzisha shuguli za uwekezaji,
na kuviwezesha vyeti vinavyotolewa na Kituo cha Uwekezaji kufanya
kazi kikamilifu.
Ø
Kutoa, kuendeleza, kujenga kurekebisha, kubadilisha, kutunza na kusimamia maeneo ya kuwekeza,
mashamba au ardhi na zana zilizopo katika maeneo, mashamba, ardhi
na kwa mujibu wa sheria zinazohusika,
kuanzisha na kusimamia kanda za kushulikia uuzaji wa bidhaa nje ya
nchi.
Ø
Kutoa na kusambaza taarifa mpya kila zinapopatikana kuhusu faida au
motisha zilizopo kwa wawekezaji
Ø
Kuandaa na kusadia shughuli za kuinua wawekezaji wa hapa wazawa ambazo
ni muhimu katika kuwatia moyo
na kuongeza wawekezaji wazawa pamoja na mipango ya
kuanzisha makampuni ya biashara.
Msaada
wa Kuanzisha Makampuni
Kituo
kitasaidia wawekezaji kuanzisha makampuni au kuyasajili kwa
kufuata hatua zituatazo
q
Kuanzisha au kusajili kampuni
q
Kujaza fomu za kodi
q
Kujaza fomu za usajili wa kuwekeza na uhamiaji
q
Kumsaida mwekezaji kupata
leseni, vibali, nyenzo au huduma anazohitaji katika shughuli zake
za kuwekeza.Endapo makabrasha yote muhimu yatawasilishwa kituoni
kama yanavyotakiwa, kituo kinaweza kukamilisha taratibu za maombi
katika siku kumi na nne.
Sheria
za Uwekezaji
Sheria
ya Uwekezaji ya Mwaka 1997
Wawekezaji, wote, wazawa na wageni ambao wana Cheti cha Motisha
kinachotolewa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania chini ya Sheria ya
Uwekezaji ya mwaka 1997, wana haki ya kufaidika na vifungu vya
Sheria ya Kodi ya Mapato ya Mwaka 1973, Sheria ya Kodi ya Ongezeko
la thamani ya mwaka 1997 na Sheria
ya Ushuru wa Forodha ya mwaka 1976.
Sheria
ya Kodi ya Mapato ya mwaka 1973
Katika kuhesabu mapato na
faida katika biashara zao wenye vyeti vya motisha wanasamehewa asilimia
mia moja (100%) ya gharama za mtaji iliyotumika katika mwaka
wowote wa mapato. Endapo mahesabu ya kipato cha jumla yataonyesha
nakisi (upungufu) kwa mwaka wowote wa mapato, kiasi hicho cha
nakisi kitasamehewa kutoka katika mahesabu ya kipato cha muhusika
kwa mwaka unaofuata wa mapato.
Kwa sekta ya madini, wawekezaji hawahitaji cheti cha motisha kupata
msamaha uliotajwa hapo juu. Aidha
wawekezaji katika sekta hii wana motisha nyingine ya posho ya
mtaji ya asilimia kumi na tano (15%). Posho hii inatolewa kwa
salio la fidia ya matumizi ya mtaji ambayo yanafanya sehemu ya
nakisi ya mwaka uliopita na iliyoruhusiwa kama punguzo kwa
muhusika mwanzoni mwa mwaka wa mapato.
Sheria
ya Ushuru wa Forodha ya Mwaka 1976
Wenye vyeti vye motisha na ambao wamewekeza kwenye sekta zilizopewa
kipaumbele kwa madhumuni ya kuimua sekta ya uwekezaji, kufuata na
kifungu cha nne cha Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997, watatozwa
ushuru wa forodha wanapoingiza zana za mitaji kwa kiwango cha
asilimia tano (5%).
Wanaowekeza katika sekta za miundombinu ya kiuchumi (ikiwa pamoja na
ujenzi wa barabara na madaraja, reli, viwanja vya ndege,
uzalishaji wa umeme, mawasiliano ya simu, huduma za maji na
nyinginezo zinazofanana na hizo) na katika sekta ya kanda ya
usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi,
hawatatozwa ushuru wanapoingiza zana za mitaji kutoka nje
ya nchi.
Wawekezaji wanajishughulisha na madini ambao hawajaanza uzalishaji wa
kibiashara, wana haki ya kuingiza nchini bila kulipa ushuru aina
zote za baruti, mafuta, vifaa vya viwanda na mahitaji mengine,
mashine, magari, na vifaa vingine kwa matumizi ya shughuli za
uchimbaji na utafutaji madini tu. Endapo watakuwa wamekwisha anza
shughuli za Kibiashara, watalipa ushuru wa forodha kwa kiwango
kisichozidi asili mia tano (5%).
Sheria
ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya Mwaka 1997
Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa uingizaji nchini wa zana za kuzalishia
mali, unaofanywa na wafanyabiashara waliosajiliwa, inaahirishwa na
itahesabiwa katika mapato watakapoanza uzalishaji wa kibiashara.
Sheria
ya Ushuru wa Forodha ya Mwaka 1976
Wakati wa ujenzi makampuni yaliyoruhusiwa wanasamehewa kulipa ushuru wa
forodha na uingizaji bidhaa na kodi nyingine zinazofanana na hizo
kwa kuingiza mashine, vipuri, mali ghafi, mafuta, magari na vifaa
vingine na ambavyo
vitatumika kwa mradi wa ujenzi.
Mali ghafi kwa shughuli za majaribio pamoja na zana nyingine
zinazoingizwa kutoka nje ya nchi ambao ni muhimu kwa matumizi ya
wataalamu wa kigeni vitasamehemewa kodi ya uingizaji bidhaa.
Sheria
ya Kodi ya Mapato ya mwaka 1973
Katika
kuhesabu jumla ya mapato, unatolewa msamaha wa asilimia
ishirini na tano (25%) ya jumla matumizi ya mtaji. Makampuni
ambayo yataonyesha
yao ya kutaka kuwekeza zaidi huko
kutokana na faida itayopatikana katika miaka mitatu ya
mwanzo baada ya kupata kibali cha kuwekeza huko Zanzibar, faida
hiyo inayotaka kuwekezwa tena itasamehemewa kodi ya mapato ya
Kampuni.
|