Kanuni na Masharti

Mtu yeyote anayefikia Tovuti Kuu hii (mtumiaji) anawajibika, na kukubali, kanuni na masharti yaliyowekwa katika notisi hii ya kisheria. Iwapo mtumiaji hataki kubanwa na kanuni na masharti haya, mtumiaji huyo hatatakiwa,  (onyesha, hatatumia, hata hawilisha (hatapakua) au vinginevyo kunakili au kusambaza matini/maudhui yaliyomo kwenye Tovuti kuu hii.

Matumizi na haki miliki
Watumiaji wanaweza kuangalia, kunakili, kupakua kwenye kinakilia, kuchapa na kusambaza matini ya Tovuti Kuu hii, au sehemu yoyote ya matini, kwa taarifa zilizo za kibiashara au kwa madhumuni ya marejeo tu.

Watumiaji wanashauriwa kuhakiki taarifa yoyote kwenye  Idara ya Serikali inayohusika, au vyanzo vingine, na kupata ushauri wowote wa kitaalamu unaofaa kabla ya kutumia taarifa iliyotolewa kwenye Tovuti Kuu ya Serikali au Mamlaka ya Serikali Mtandao kwa vyovyote vile hatahusika na gharama yoyote, hasara au madhara yatakayotokana na kutumia data, inayotokana  au kuhusiana na kutumia Tovuti Kuu ya Serikali.

Haki zote za maadili na haki nyingine zozote za Tovuti Kuu ya Serikali au chombo kingine chochote cha kisheria ambacho kwamba matini yake yamo ndani ya Tovuti Kuu hii ambayo haikutolewa kwa madhumuni hayo, zimehifadhiwa.

Angalizo la Dhamana
Taarifa iliyomo ndani ya Tovuti Kuu hii imekusudiwa kukupa taaria ya jumla tu kuhusu mada mahususi au mada mbalimbali na haikukamilisha kabisa mada hiyo/hizo.

Viungo kwenda tovuti nyingine zilizojumuishwa ndani ya Tovuti Kuu hii, vimetolewa kwa kurahisisha matumizi kwa wananchi tu. Mamlaka ya Serikali Mtandao haiwajibiki na matini au kuaminika kwa tovuti zilizounganishwa.

Hatukuhakikishii upatikanaji wa kurasa zilizo unganishwa wakati wote.

Taarifa zilizoelezwa ndani ya Tovuti Kuu hii zinaweza kunakiliwa bure baada ya kupata idhini kwa kutotumia barua pepe au Kiungo cha “maoni” kinaweza kutumika. Hata hivyo taarifa ni lazima zinakiliwe kwa usahihi na zisitumike kukashifu, kushushia hadhi  au kutukana au kupotosha.

Kila wakati taarifa inapochapishwa au kupewa watu au vyombo vingine, chanzo ni lazima kitajwe waziwazi. Hata hivyo idhini ya kunakili taarifa haitahusu taarifa yoyote ile, iliyo bainishwa kuwa ni haki miliki ya mtu wa tatu. Idhini ya kunakili au kutoa tena kwa namna yoyote ile ni lazima itolewe na idara / mwenye haki miliki anayehusika.

Mpangilio