Kilimo

Muhtasari

Nchini Tanzania, Sekta ya Kilimo ni muhimili wa maendeleo ya uchumi. Sekta hii inachangia kiasi cha nusu ya pato la Taifa, robo tatu ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na chanzo cha chakula pamoja na utoaji wa fursa za ajira zaidi ya 75% ya Watanzania. Kilimo kina uhusiano na sekta zisizo kuwa za kilimo kupitia uhusiano wa usafishaji kwenda kwenye usindikaji wa mazao ya kilimo, matumizi na uuzaji nchi za nje;Inatoa malighafi kwa viwanda na soko kwa bidhaa zilizotengenezwa. Tanzania inazalisha takribani 97% ya mahitaji yake ya chakula. Uzalishaji wa mazao ya chakula unatofautiana mwaka hadi mwaka kutegemea kiasi cha mvua kilichopatikana.

Maendeleo ya kilimo yamekuwa chini ya Serikali/fedha za umma kwa kipindi kirefu. Hata hivyo marekebisho ya uchumi kwa jumla yamekuwa na yanaendelea kuwa na matokeo ya muhimu kwenye sekta ya kilimo. Marekebisho ya kiuchumi yamesababisha kufunguka sekta hiyo kwa uwekezaji binafsi katika uzalishaji na usindikaji , uagizaji pembejeo za kutoka nchi za nje na usambazaji na masoko ya kilimo. Serikali imebaki na kazi ya usimamizi na usaidizi wa umma na dhima ya uwezeshaji.

Taarifa iliyojumuishwa kwenye sehemu hii itakusaidia mwananchi kuelewa kuhusu upimaji wa udongo na rutuba, uhifadhi, masoko na upangaji wa bei, ulishaji wa mifugo, mbolea na viuatilifu, taratibu bora kwenye kilimo cha kutumia mbolea ya asili, ufugaji wa nondo wa hariri, kilimo cha bustani, ufugaji wa samaki, kilimo cha maua na namna ya kupata mikopo ya kilimo na ruzuku. Kwa taarifa zaidi tembelea  Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika 

Programu zinazotekelezwa na Wizara ya Kilimo

i. Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II)

Mpango huu unalenga kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo (mazao, mifugo na uvuvi) kuongeza uzalishaji, biashara na kipato cha mkulima wa hali ya chini ili kuboresha hali ya maisha, usalama wa chakula na lishe na mchango katika Pato la Taifa.

Mkakati wa utekelezaji wa mpango huu ni kuwabadilisha na kuwafanya  wakulima wadogo wadogo kulima kibiashara kwa kuimarisha na kuamsha vichochezi vya sekta na kuwawezesha wakulima wadogo kuongeza uzalishaji katika bidhaa lengwa ndani ya mifumo ya uzalishaji endelevu na kuanzisha uhusiano endelevu wa soko kwa ajili ya ushindani wa kibiashara na maendeleo ya mnyororo wa thamani.

ii.    AGRI-CONNET

Hii ni programu inayofadhiliwa na Umoja wa nchini za Ulaya inayolenga katika kukuza uchumi, kukuza maendeleo ya sekta binafsi na kutengeneza ajira katika sekta ya kilimo, na kuongeza usalama wa chakula na lishe nchini.https://www.kilimo.go.tz/programmes/view/agri-connect

iii.Building a Better Tommorow
 

Dondoo za Bajeti 2022/2023

  • Wizara imetenga jumla ya Sh751 bilioni sawa na asilimia 155.34 ikilinganishwa na Sh294 bilioni za bajeti ya mwaka 2021/2022 wa fedha.

 

  • Bajeti ya sekta hii imepanda karibu mara tatu na kutenga fedha zaidi katika utafiti na umwagiliaji.

 

  • Sh631.5 bilioni ambazo ni takriban  ya asilimia 84 ya bajeti ya wizara zitagharamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

 

  • Sehemu kubwa ya fedha hizo imetengwa kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji, miundombinu ya kuhifadhi mazao, kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao, kuimarishwa kwa utafiti wa kilimo, uzalishaji wa mbegu na ruzuku.

 

  • Bajeti ya umwagiliaji pekee itaongezeka kutoka Sh46.5 bilioni hadi Sh361.5 bilioni katika mwaka huu wa fedha huku bajeti ya utafiti wa kilimo ikiongezeka kutoka Sh11.63 bilioni hadi Sh40.73 bilioni.

 

  • Wizara ina mpango wa kumwagilia hekta milioni 1.2 ifikapo mwaka 2025 kwa lengo la kuboresha kilimo cha umwagiliaji.

 

  • Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kujenga skimu mpya 25 za umwagiliaji zenye ukubwa wa hekta 53,234 katika mwaka wa fedha wa 2022/2023.

 

  • Mbali na ongezeko la bajeti ya umwagiliaji, uzalishaji wa mbegu na utafiti wa kilimo, Serikali pia itaongeza bajeti ya ujenzi wa ghala kutoka Sh2.02 bilioni hadi Sh25.16 bilioni huku ile ya huduma za ugani ikiongezeka kutoka Sh11.5 bilioni hadi Sh15. bilioni.

 

  • Sekta ndogo ya mazao ilipanuka kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 4.8 katika kipindi tunachotathminiwa.

 

  • Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2022/2023 inalenga kujenga msingi imara wa ukuaji wa sekta ya kilimo kwa kiwango cha asilimia 10 ifikapo 2030. Kiwango hicho cha ukuaji kitachangia kupunguza umasikini kwa asilimia 50. 

Huduma za Ugani za Kilimo

Huduma za ugani ni muhimu sana katika kusaidia kupunguza umaskini vijijini na ushindani wa soko kwa ajili ya kilimo cha biashara katika soko la ndani na soko la kimataifa. Huwawezesha wakulima kuongeza mazao na tija kwa upataji taarifa ya huduma za masoko na huduma nyingine za msaada muhimu kwa maendeleo ya kilimo. Mageuzi ya huduma za ugani za kilimo ni muhimu ili kutoa zana sahihi, maarifa na stadi pamoja na kuhakikisha kuwa wakulima wanafuata Kanuni Bora za Kilimo. Mahitaji ya Taifa ya maofisa ugani ni 15,082 ili waweze kuhudumia wakulima katika kila kata na kijiji kwa kuleta ufanisi na tija. Mpaka sasa wapo maofisa ugani 7,974 ambao ni takribani 50% ya jumla ya mahitaji. Juhudi ziko mbioni kuwafunza na kuwapangia wafanyakazi wanaohitajika

Kilimo cha Bustani

Tasnia ya kilimo cha bustani ina umuhimu mkubwa kwa uchumi wa sekta ya kilimo.

Kwa taarifa zaidi tembelea https://www.kilimo.go.tz/resources/view/mkakati-wa-kuendeleza-horticulture

 

Usimamizi na Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Kilimo

 USIMAMIZI NA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI YA KILIMO

Wizara ya Kilimo kupitia Idara ya Usimamizi na Mipango  ya Matumizi ya Ardhi ya Kilimo inatoa huduma mbalimbali kama zifuatavyo:-https://www.kilimo.go.tz/resources/view/usimamizi-na-mipango-ya-matumizi-ya-ardhi-ya-kilimo 

Mpangilio