Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alianzisha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Tangazo la Serikali Na.782 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali la tarehe 22 Novemba, 2021 kama ilivyofanyiwa marekebisho kwa Notisi ya Serikali ya tarehe 17 Januari, 2025
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ina Majukumu yafuatayo:
Dira
Kuwa na Taifa linalohabarishwa kikamilifu, lililoshamilika kiutamaduni, lenye kazi bora za Sanaa na lenye umahiri katika michezo.
Dhima
Kuendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji stahiki wa Habari, kukuza utamaduni, Sanaa na michezo kwa lengo la kuleta maendeleo ya jamii kiuchumi.