Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alianzisha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Tangazo la Serikali Na.782 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali la tarehe 22 Novemba, 2021 kama ilivyofanyiwa marekebisho kwa Notisi ya Serikali ya tarehe 17 Januari, 2025

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ina Majukumu yafuatayo:

  1. Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Sera za Sekta ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo.
  2. Kuendeleza, kuwezesha na kuratibu masuala ya kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara.
  3. Kusimamia na kuratibu Maendeleo ya Sekta ya Habari nchini.
  4. Kusimamia na kuratibu Maendeleo ya Utamaduni nchini.
  5. Kusimamia na kuratibu Maendeleo ya Sanaa nchini.
  6. Kusimamia na kuratibu Maendeleo ya Michezo nchi.
  7. Kusimamia utendaji wa Taasisi, Mashirika ya Umma, Wakala, Miradi na programu zilizo chini ya Wizara.

Dira

Kuwa na Taifa linalohabarishwa kikamilifu, lililoshamilika kiutamaduni, lenye kazi bora za Sanaa na lenye umahiri katika michezo.

Dhima

Kuendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji stahiki wa Habari, kukuza utamaduni, Sanaa na michezo kwa lengo la kuleta maendeleo ya jamii kiuchumi.

 

Mpangilio