Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

VIPAUMBELE VYA WIZARA KWA MWAKA 2023/24

  1. Kuratibu afua za kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake kiuchumi (Generation Equality Forum - GEF);
  2. Kuratibu utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA);
  3. Kutekeleza Mpango wa Taifa wa Kuhamasisha na Kusimamia Maendeleo Ngazi ya Msingi wa mwaka 2022/23 - 2025/26 (Bottom Up);
  4. Kukuza ari ya jamii kushiriki katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo;
  5. Kutambua na kuratibu Makundi Maalum wakiwemo wafanyabiashara ndogondogo ili kuboresha mazingira ya biashara zao;
  6. Kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii, Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii;
  7. Kuratibu utoaji wa huduma za msingi kwa watu wenye mahitaji maalum ikiwemo huduma za msaada wa kisaikolojia kwa manusura wa majanga mbalimbali na makundi mengine yenye uhitaji katika jamii;
  8. Kuratibu na kuwezesha upatikanaji wa haki za watoto na huduma za ustawi wa jamii kwa wazee;
  9. Kuimarisha mifumo ya malezi, ulinzi na maendeleo ya watoto na familia; na
  10. Kuimarisha utendaji kazi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ili mchango na ushiriki wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika maendeleo ya Taifa uweze kutambulika na kuwa na tija kwa jamii. Zaidi visome /www.jamii.go.tz 

HISTORIA YA WIZARA

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum iliundwa tarehe 8 Januari, 2022 lililotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uundwaji wa Wizara hii ulitokana na uamuzi wa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wa kutenganisha iliyokuwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kuunda Wizara zinazojitegemea kulingana na majukumu yake.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina Idara saba (7), Vitengo sita (6), Taasisi na Vituo vya Ustawi kama ifuatavyo:-

        ​​​​​​​Idara za Kiutendaji

  1. Idara ya Maendeleo ya Jamii;
  2. Idara ya Ustawi wa Jamii;
  3. Idara ya Maendeleo ya Jinsia;
  4. Idara ya Maendeleo ya Mtoto; na
  5. Idara ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

​​​​​​​         Idara Wezeshi

  1. Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu; na
  2. Idara ya Sera na Mipango.

​​​​​​​         Vitengo

  1. Kitengo cha Fedha na Uhasibu;
  2. Kitengo cha Ununuzi na Ugavi;
  3. Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani;
  4. Kitengo cha Huduma za Sheria;
  5. Kitengo cha Mawasiliano Serikalini; na
  6. Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

 

    Taasisi Zinazosimamiwa na Wizara

Taasisi mbili zinazojitegemea zilizo chini ya Wizara ni:-

  1. Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru; na
  2. Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kijitonyama.

​​​​​​​Taasisi Nyingine Zilizo chini ya Wizara

Wizara inasimamia Taasisi zinazowajibika moja kwa moja kwa Katibu Mkuu katika utekelezaji wa majukumu yake. Taasisi hizo zinatoa elimu kuhusu maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii pamoja na huduma za ustawi wa jamii. Taasisi hizo ni:-

        Vyuo nane vya Maendeleo ya Jamii;

  1. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha,
  2. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba,
  3. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole,
  4. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale,
  5. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Misungwi,
  6. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare,
  7. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Mabughai, na
  8. Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli.
  1.            Makazi ya Wazee 14;
      1. Makazi ya Wazee Kibirizi,
      2. Makazi ya Wazee Magugu,
      3. Makazi ya Wazee Ipuli,
      4. Makazi ya Wazee Njoro,
      5. Makazi ya Wazee Mwanzange,
      6. Makazi ya Wazee Sukamahela,
      7. Makazi ya Wazee Kolandoto,
      8. Makazi ya Wazee Bukumbi,
      9. Makazi ya Wazee Kilima,
      10. Makazi ya Wazee Nunge,
      11. Makazi ya Wazee Nyabange,
      12. Makazi ya Wazee Nandanga,
      13. Makazi ya Wazee Fungafunga, na
      14. Makazi ya Wazee Misufini.
  2. Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini – Dar es Salaam na Makao Mapya ya Taifa ya Watoto Kikombo – Dodoma;
  3. Shule ya Maadilisho Irambo - Mbeya;
  4. Mahabusu sita (6) za Watoto;
      1. Mahabusu ya Watoto Arusha,
      2. Mahabusu ya Watoto Kilimanjaro,
      3. Mahabusu ya Watoto Mbeya,
      4. Mahabusu ya Watoto Tanga,
      5. Mahabusu ya Watoto Dar es Salaam, na
      6. Mahabusu ya Watoto Mtwara (inahitaji ukarabati).
  5. Makazi ya Wazee Yaliyofungwa;
  6. Makazi ya Wazee Ngehe,
  7. Makazi ya Wazee Mkaseka, na
  8. Makazi ya Wazee Chazi.

DIRA

Kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

DHIMA

Kukuza maendeleo ya jamii, usawa wa jinsia, haki za wazee na watoto, ustawi wa jamii na ushiriki bora wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni, Mikakati na Miongozo mbalimbali.  https://www.jamii.go.tz/pages/historical-background

 

ORODHA YA TAASISI ZA USTAWI WA JAMII

SN

NAME OF INSTITUTION

REGION

1  

KIKOMBO NATIONAL CHILDRE’S HOME

 

DODOMA

2       

KURASINI NATIONAL CHILDRE’S HOME

 

DAR ES SALAAM

3

ILONGA CHILDRE’S HOME

 

MOROGORO

4

TEMEKE JUVINILE COURT

 

DAR ES SALAAM

5   

KISUTU JUVINILE COURT

 

DAR ES SALAAM

6

 MBEYA JUVINILE COURT

 

MBEYA

7   

UPANGA RETENTION HOME

 

DAR ES SALAAM

8     

ARUSHA RENTATION HOME

 

ARUSHA

MTWARA RENTATION HOME

 

MTWARA

10  

MBEYA RENTATION HOME

 

MBEYA

11   

KILIMANJARO RENTATION HOME

 

KILIMANJARO

12  

TANGA RENTATION HOME

 

TANGA

13

IRAMBO APPROVED SCHOOL

 

MBEYA

14

NUNGE ELDERLY HOME

 

DAR ES SALAAM

15

BUKUMBI ELDERLY HOME

 

MWANZA

16

FUNGAFUNGA ELDERLY HOME

 

MOROGORO

17

SUKAMAHELA ELDERLY HOME

 

SINGIDA

18

IPULI ELDERLY HOME

 

TABORA

19

KOLANDOTO ELDERLY HOME

 

SHINYANGA

20

KILIMA ELDERLY HOME

 

KAGERA

21    

MISUFINI ELDERLY HOME

 

TANGA

22

MWANZAGE ELDERLY HOME

TANGA

23    

LITETE MINGOYO ELDERLY HOME

 

LINDI

24  

NYABANGE ELDERLY HOME

 

MARA

25

KIBIRIZI ELDERLY HOME

 

KIGOMA

26

MAGUGU ELDERLY HOME

 

MANYARA

27

NJORO ELDERLY HOME

 

KILIMANJARO

28

CHAZI ELDERLY HOME

 

MOROGORO

29

NANDANGA ELDERLY HOME

 

LINDI

Miongozo ya Mabaraza ya Watoto na uanzishwaji wa Madawati ya Watoto

Miongozo ya Mabaraza ya Watoto na uanzishwaji wa Madawati ya Watoto katika Shule za Msingi na Sekondari imezinduliwa Siku ya Mtoto wa Afrika ikiwa ni hatua muhimu katika kukabiliana na kadhia ya ukatili kwa kundi hilo ndani ya jamii. Kuzinduliwa kwa miongozo hiyo ni hatua muhimu katika kusukuma ajenda ya kupinga ukatili hususan kwa kundi hilo la watoto.

Watoto nchini wamekuwa wakipitia ukatili mbalimbali ikiwemo wa mitandaoni, hivyo Serikali kwa kushirikiana na wadau na imeandaa miongozo kwa Wanafunzi, Walimu pamoja na Wazazi ili iwe msaada katika malezi na makuzi ya watoto wetu” alisema Dkt. Gwajima.

 Serikali kupitia Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 inatambua Haki tano (5) za Msingi za Mtoto ambazo ni Haki ya Kuishi, Kulindwa, Kuendelezwa, Kushiriki na haki ya Kutobaguliwa hivyo kuzinduliwa kwa mongozo ni chachu ya kuongeza mapambano ya kumlinda Mtoto. Miongozo hiyo itapelekwa kwenye Shule za Msingi na Sekondari pamoja na Vyuo vya kati, kwenye Madawati ya ulinzi wa Mtoto na Mabaraza ya Watoto ambayo yanakwenda kuanzishwa nchi nzima ili iwe ni fursa kwa watoto kujadiliana na kueleza madhila yanayowasibu.

Serikali pamoja na Wadau baada ya tafiti zake waliona umefika wakati kwa watoto kupatiwa Miongozo itakayowasaidia uendeshaji wa Mabaraza yao. Wazazi na walezi kote nchini wanatakiwa kuwaruhusu watoto kujiunga na kushiriki katika mabaraza ya Watoto ili kutoa fursa kwa wao wenyewe kubainisha changamoto zinazowakabili.

Chimbuko la Siku ya Mtoto wa Afrika ni azimio la Umoja wa nchi za Afrika (OAU) la mwaka 1991 lililokuwa na lengo la kuwaenzi Watoto kutoka shule mbalimbali za nchini Afrika Kusini hususani Kitongoji cha Soweto waliouawa kinyama na Polisi wa Serikali ya Makaburu tarehe 16 Juni,1976. Watoto hao wanaokadiriwa kufikia 2000 waliuawa wakati wanaandamana kupinga elimu ya kibaguzi dhidi ya watoto wenye asili ya kizungu.

Mpangilio